Tuesday, September 16, 2008

KUFA

Kwa nini watu kwanza tunazaliwa halafu tunakufa. Wengine wanaishi dakika, saa, siku, miezi, mwaka, miaka na miaka. Mara nyingi nimekuwa nikiwaza neno KUFA lazima itakuwa ni pumziko la amani sana kulala kwenye lile sanduku giza na hali tulivu hakuna anayekusumbua peke yako.



Unajua kama una ndugu, jamaa na marafiki ambao hawakujali kwa nini kuishi peke yako hapa duniani wakati kuna uwezo wa kuwa upweke Kaburini. Afadhali kabisa kufa. Haya ni mawazo yangu.



Kama ilivyoandikwa: Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi akampulizia puani PUMZI YA UHAI na mtu yule akawa NAFSI hai.

Kufa ni kama kulala usingizi usio na ndoto. Yesu alifundisha hivyo.

Baada ya kufa ubongo unaharibika hauwezi kujua , wala kukumbuka kitu chochote. Hisia zote za moyo za kibinadamu hukoma kabisa mtu anapoishi.

"Kama mimi niishivyo, atangaza Bwana Mungu,..... kila ROHO ILIYO HAI(LIVING SOUL) ni mali yangu....... ROHO YULE ATENDAYE DHAMBI NDIYE ATAKAYEKUFA." Ezekieli 18;3-4.

Swali:- Kwa nini yesu alikufa na akafufuka na sio sisi wengine "wanadamu"?