Sunday, August 31, 2008

AGOSTI 31, 2008 NYUMBANI(KUNYUMBA)

Peramiho kwa mbali






Kanisa la Peramiho




Angalien jinsi kunavyopendeza au mnasemaje. msione aibu jamani ni kuzuri. Karibuni sana Ruvuma Peramiho.

Friday, August 29, 2008

AGOSTI 30, 2008 Umuhimu wa hadithi Tanzania yetu

Wote tunakumbuka/tunajua kuwa:-

Wakati wa ukoloni elimu ilikuwa ni ya wachache walioteuliwa tu.

Lengo kubwa la taratibu za elimu ya wakoloni ni kuzalisha makarani na wasaidizi wa utawala wa kiingereza.

Mara tu baada ya Uhuru mwaka 1961 taratibu za elimu zilibadilishwa ili kufuata mazingira na mahitaji ya watanzania ambao karibu 90% waliishi vijijini na mikoani. Kiingereza kilikuwa ndiyo lugha iliyotumika kufundishia wakati ule wa utawala wa kikoloni.

Kiswahili kilianza kutumika katika shule za msingi mnamo mwaka 1969. Matokeo ni kwamba vitabu vya masomo kwa kiswahili vilikuwa vichache.

Kwa vile wakoloni walitawala basi Tanzania kwa muda mrefu ilikuwa bado ingali katka hali mbaya ya uchumi, haikuwezekana kufanyika mengi. Katika baadhi ya mashule, walimu walikuwa wanawaalika wazee waje kusimulia watoto hadithi na visa vya kale. Wazee walitambuliwa kama maktaba na hazina ya ujuzi uliojengeka kwa mila za masimulizi.

Tanzania ina makabila karibu 129 mbalimbali ambayo kati yao kuna lugha na mila mbalimbali tofauti sana. Kwa hiyo kukusanywa kwa hadithi toka makabila hayo yote na kufasiriwa kwa kiswahili, kumefanya hadithi ziwe ni msingi mmoja wa mila na utamaduni wa kitanzania. Tutumaini hadithi zote zilizosimuliwa na wazee wetu zimehifadhiwa la sivyo tutakuwa tumepoteza utajiri mkubwa wa mila na ujuzi kupotea.


kumbukumbu kutoka:- kitabu cha hadithi na visa kutoka Tanzania

AGOSTI 29, 2008 KUMBUKUMBU/NDOTO

Tosamaganga Seminary





Baba yangu amesoma hapa alitaka kuwa padre. kwa hiyo mimi ningekuwepo leo.



Misha ya utawa




Leo nimekuwa najiuliza je ningeweza kweli kuishi maisha ya utawa?

Thursday, August 28, 2008

AGOSTI 28, 2008 WIMBO WA TAIFA

Usiku mzima leo sijalala kisa nilikuwa nimekumbuka sana wakati nasoma shule na msingi na kuimba wimbo huu:-


Tanzania Tanzania,
Nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanzania,
Jina lako ni tamu sana,
Nilalapo nakuota wewe,
Niamkapo ni heri mama wee,
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote.


Tanzania Tanzania,
Ninapokwenda safarini,
Kutazama maajabu,
Biashara nayo makazi,
Sitaweza kusahau mimi,
Mambo mema ya kwetu kabisa
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote


Tanzania Tanzania,
Watu wako ni wema sana,
Nchi ngingi zakuota,
Nuru yako hakuna tena,
N wageni wakukimbilia,
Ngome yako imara kweli wee,
Tanzania Tanzania
Heri yako kwa mataifa.



Nchi nzuri Tanzania,
Karibu wasio kwao,
Wenye shida na taabu,
Kukimbizwa na walowezi,
Tanzania yawakaribisha,
Mpigane kiume chema wee,
Tanzania Tanzania
Mola awe nawe daima.

Wednesday, August 27, 2008

Tuesday, August 26, 2008

AGOSTI 26,2008 Wabunge wamzomea Mugabe.



Wabunge wa chama kikuu cha upinzani cha MDC nchini Zimbabwe wamezomea Rais Robert Mugabe alipofungua rasmi bunge miezi mitano baada ya uchaguzi uliokuwa na utata.
Wabunge hao walihanikiza kwa kupiga makelele wakati Bwana Mugabe, alipokuwa akiorodhesha mafanikio ya serikali yake "Umeua watu, kamwe hatutakusahau"
Mwanzo wa hutuba yake, Bwana Mugabe amesema kuna matumaini makubwa mazungumzo ya kugawana madaraka yatafanikiwa.
Upande wa upinzani ulitaka bunge lisifunguliwe hadi mazungumzo yaliyokwama yatakapopatiwa ufumbuzi.
Awali chama cha MDC kilitishia kususia hutuba ya Rais Mugabe, kwa vile hawautambui utawala wa Mugabe.
Kufuatia uchaguzi mkuu wa mwezi Machi, chama cha Mugabe cha Zanu-PF kilipoteza wingi wa viti bungeni kwa mara ya kwanza tangu Zimbabwe ilipopata uhuru mwaka 1980.
Katika hutuba yake Bwana Mugabe ameeleza kusikitishwa na vurugu za kisiasa zilizotokea wakati wa uchaguzi mwaka huu na kuvitupia lawama vyama vyote vya siasa.

AGOSTI 26,2008 MIMI NIKIWA NAISHI KINGOLI/LITUMBADYOSI

Binadamu tuko tofauti kuna wengine wanasahau upesi na wengine kama mimi. Ni hivi kuna jambo moja, ambalo mimi SITALISAHAU nilikuwa miaka 10 labda. Baba na mama walikwenda hospital Litembo. Na mimi na kaka zangu tulibaki kwa (babu) baba mkubwa. Huyu baba mkubwa alikuwa na watoto wa kike 6 na huyu mkubwa aliitwa Maria. Siku moja jumapili;- Nilimwomba dada Maria kanga kwani mimi nilikuwa sina ALININYIMA na kuniambia kwa nini baba yangu ambaye ni mwalimu asininnunulie. Kwani wakati ule nilikuwa mtoto wa kike peke yangu. Naye alisema, upo peke yako mtoto wa kike na wazazi wako wanashindwa hata kukununulia kanga.(Mwana mdala nga veve vishindwa kukugulila nyula).Kilugha Siku ile nililia sana, mpaka sasa roho bado inaniuma. Sikujua kama binadamu wanaweza kuwa wakatiri kiasi hiki, na hasa ukizingatia yeye alikuwa dada yangu. Kwa mimi ni vigumu kuelewa. Tokea siku ile sijawa na mawasiliano naye natumaini hata yeye anakumbuka alinifanyia nini. Lakini sidhani kwani waswahili wanasema mtendaji hakumbuki ila mtendewa ndiye anayekumbuka. Mimi ni mtu mmoja ambaye kwa ujumla ni mvivu. Nina maana kuhusu mambo ya kazi ngumu hasa nilipokuwa mdogo.Kule kingoli maisha yalikuwa magumu kulima mpunga na pia karanga na mihogo. Nakumbuka kila wakati mimi nilikuwa wa mwisho wakati tulikuwa shambani.Yaani walikuwa wananiachia/ruka matuta.Mazao ambalo tulikuwa tunalima sana ni karanga na mpunga tangu asubuhi mpaka mchana. Halafu kule kingoli tulikuwa tunakula sana ugali wa muhogo na kwa kuwa sisi tulihamia kule, tulikuwa hatuna shamba la mihogo. Kwa maana hiyo ilibidi tununue, ndugu yangu huko tulikonununu kulikuwa mbali mnatembe mpaka miguu inauma. Tulikuwa tunachimba, kumenya kabisa ili uzito upungue. Baada ya hapo kurudi na mzigo kichwani na jua linawaka. Kufika nyumbani kutua mzigo, kuandaa chakula cha mchana na kula. Kupumzika kidogo kisha kuanza kazi ya kuchotelea maji ya kulowekea ile mihogo. Kwani kulikuwa hakuna maji ya bomba, tulikuwa tunachota kisimani. Jamani kweli maisha ni safari ndefu, nina maana kuna watu wengine hawatanielewa nini ninachokisema. Kwa kusema kweli maisha yangu hayajawa afadhali nimeendelea kuteseka mpaka leo. Nadhani mungu alipanga niwe mtu wa mateso mpaka siku ya mwisho.

Monday, August 25, 2008

AGOSTI 25, 2008 SALAMU KUTOKA MIKUMI




Katika picha ni Camilla na Erik Mwaka jana wakati tupo Tanzania kuwasalimia babu, wajomba,mama mdogo na pia ndugu wengine. Hapa ni kituo cha kwanza Mikumi. Pia tunapenda kutoa salamu kwa rafiki yetu Emanuel Lazarus.

Ujumbe watoto tupendane.

Sunday, August 24, 2008

AGOSTI 24,2008 SALAMU KUTOKA KWA YASINTA NGONYANI

Did anyone ever tell you how important you make others feel. Somebody out there is smiling about love that is so realy.

Did anyone ever tell you just how much they like you? well, my dearest friend today Iam telling you.

I believe that without a friend you are missing out on a lot!!!

Have a nice day, and I`m glad we are friends!!!!

FRIENDSHIP IS CONTINUOUS HOPE YOU HAVE A GREAT DAY

Saturday, August 23, 2008

AGOSTI 23, 2008 Esther Wahome









Nampenda sana dada Esther Wahome sikiliza halafu niambee kwa nini? Yeye ni (my Idol)

AGOSTI 23,2008 MIMI NDIVYO NILIVYO

Udadisi;- Watu wengi wamechoka na mimi kutokana na udadisi wangu, maswali yangu pia. Wanasema huwa hawapati jibu waulizapo swali/maswali. Badala ya kupata jibu, wanapata swali pia. kama vilw KWA NINI? Ni kweli huwa nafanya hivi, sio kwamba nataka kuwatesa wao hapana ila ndivyo nilivyo au niseme ndivyo nilivyozaliwa. Na nimekwisha zoea ila sasa wengi wanaona kero sana. Je ni tabia mbaya kufanya hivyo? Nisaidieni wasomaji.

Friday, August 22, 2008

AGOSTI 22,2008 ERIK NA YASINTA KATIKA MAZOEZI YA KUKIMBIA


Leo nimeamua kumchukua na kijana wangu kwenda kufanya mazoezi ya kukimbia tukiwa tumevalia T-shirt za kutoka TZ. Je? unafikiri nani alimshinda nani. Kuna zawadi inamsubiri atayejibu vizuri.

Thursday, August 21, 2008

AGOSTI 21/8 2008 NITAKAPO KUWA MZEE



Huyu bibi nimempenda sana. Mungu akinijaria maisha marefu, mpaka nitakapokuwa mzee nataka kuwa kama yeye. Napenda makunyanzi yake.

Wednesday, August 20, 2008

AGOSTI 20, 2008 MAISHA,UNYANYASAJI NA ELIMU

Wote tunajua maisha ni changamoto, maisha ni mawasiliano yanayotufundisha kukuabiliana na changamoto zote. Kwa hiyo inabidi tusimame imara. Kama nilivyosema hapo mwanzoni madawa ya kulevya, inaonekana ni kishawishi kikubwa kwa wengi, ambacho inabidi tukabiliane nacho. Maisha si rahisi wakati wote, wote tunatakiwa kuwa makini na hodari ili tuweza kukabiliana na mambo mbalimbali tunayotaka katika maisha yetu. Hakuna mwingine ayaongozayo maisha yetu zaidi ya sisi wenyewe au wewe mwenyewe. Kwa hiyo inabidi kuchagua na kuamua mambo fulani fulani maishani mwako/ mwetu. Tunatakiwa kuweka malengo yetu na KUKATAA vishawishi ambavyo tunajua vitayaharibu maisha yako/yetu. Tumbumbuke wahenga walisema utavuna ulichopanda.

Halafu kuna hili jambo la unyanyasaji:- Unyanyasaji, kuna ukatili mwingi sana hapa duniani ambao zaidi ni juu ya wanawake na watoto. Hao ndio wanaopata shida zaidi. Ukatiki ni kinyume na haki za binadamu na uko ukatili wa aina mbalimbali. Kuna vipigo, matusi, kulazimishwa kufanya mapenzi, kuna baadhi ya mila potofu kama vila ndoa za lazima, kuolewa ukiwa na umri mdogo, kurithi wajane, pia ni ukatili kutahiri wanawake.

Nisisahau jambo la elimu:- Wote tunajua ujuzi ni nguvu na elimu ni ufunguo wa maisha. Hii ndiyo sababu tunaenda shuleni, ili tuweze kupata elimu na kujua mambo. Kumbuka usipokuwa na elimu nzuri huwezi kupata kazi nzuri.

Tuesday, August 19, 2008

AGOSTI 19,2008 CHOO/VYOO

Kuna watu zaidi ya 2,600 000 000 hawana choo, kati ya watu 6,000 000 000 ulimwenguni theruthi hawana choo, na 2,6000 000 000 hawana choo safi au hawana kabisa. Mambo haya yamezungumzwa na Stockholm International Water Institute (SIWI) jumamosi 16/8-08.

Tatizo hili limezidi sana kusini mwa Afrika na Bara la Asia. Imefikia mpaka mavi yapo kila mahali kama barabarani na sehemu za kupumzikia. Hatari zaidi kwani sasa vijidudu(bacteria) wanaingia kwenye mabomba ya maji safi maji ya kunywa

KUMBUKUMBU,HISTORIA


Hili ni kanisa ambalo nilibatizwa, na nimesali tangu siku ile niliyobatizwa mpaka nilipokuwa darasa la nne. Sasa nimerudi tena baada ya kupoteana kwa muda wa miaka ishirini. Kanisa hili lipo katika kijiji cha Lundo kando ya ziwa Nyasa kusini magharibi mwa Tanzania. Na kanisa hili linaitwa MAKWAI.

Monday, August 18, 2008

AGOSTI 18,2008 KUKUMBATIANA (A HUG)

Leo nimeamua kuandika swala la kukumbatiana:-

Kukumbatiana ni aina ya kugawana furaha na uchungu. Wote tunahitaji kukumbatiana kwa sababu tunajaliana. Kuanzia bibi mpaka yule umpendaye. Kukumbatiana ni kitu cha kustaajabisha (kizuri). Ni njia nzuri ya kuonyesha upendo bila kutumia maneno. Ni ajabu kuona kukumbatiana kunawapa watu furaha. Kukumbatiana kunafaa kila mahali kwa lugha zote. Kukumbatiana hakuhitaji betri. Kwa hiyo sasa inachobidi ni kuendeleza mkumbato na mpe/wape rafiki zako na yule umpendaye. Haya mimi nanza tayari sasa hivi nimesha kukukumbatia. :-)

Sunday, August 17, 2008

AGOSTI 17, 2008 KUMBUKUMBU,KUTOWEKA KWA MAMA YANGU

Mpaka leo ni miaka minne (4) imepita tangu mama yangu mpendwa Alana magnus Ngonyani aiage dunia hii. Ila kwa mimi inaonekana kama ilikuwa jana tu. Napenda kukuombea mama kwa sara hii:-


Salamu, Maria, umejaa neema,
Bwana yu nawe,
umebarikiwakuliko wanawake wote,
Na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
Utuombee sisi wakosefu,
Sasa na saa ya kufa kwetu,
Amina.


Marehemu astarehe kwa amani, Amina.




Saturday, August 16, 2008

video

Kedmon Mapena kanisa la skoghall





Nova Cantica

Agosti 16, 2008 KAMBI ZA AFRIKA KUSINI




Zaidi ya watu 60 waliuawa kutokana na ghasia dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini
Maafisa wa serikali ya Afrika Kusini wameamua kuongeza muda zaidi hadi Jumatatu, kabla ya kutoa amri ya kufungwa kwa kambi sita ambazo ziliwapokea wakimbizi nchini humo, kufuatia ghasia dhidi ya wageni mwezi Mei.
Muda huo utatoa nafasi kwa mahakama ya katiba kupata nafasi zaidi, kabla ya kutoa uamuzi wake, baada ya makundi ya kutetea haki za binadamu kupinga hatua ya kutaka kuzifunga kambi hizo.
Mamlaka ya serikali katika mkoa wa Gauteng inaeleza kwamba ni salama sasa kwa wageni kuweza kurudi katika makazi yao.
Kambi hizo zilianzishwa mwezi Mei, baada ya zaidi ya watu 60 kuawa, na maelfu kupoteza makao yao, kufuatia ghasia dhidi ya wageni.
Mapema wiki hii, jaji mmoja wa mahakama kuu alikataa rufaa kutoka kwa makundi yanayotetea haki za binadamu, ambayo yanasema kwamba kuzifunga kambi hizo ni kuwanyima haki wakimbizi wanaoishi humo.
Awali mahakama ya katiba ilikuwa inatazamiwa kutoa uamuzi Ijumaa.
Ghasia hizo dhidi ya wageni ndizo zilizokuwa mbaya tangu siku za uongozi wa ubaguzi wa rangi uliokomeshwa mwaka 1994.
Zilianza katika mtaa mmoja kaskazini mwa Johannesburg, na kuenea kote nchini.
Walioshambuliwa walilaumiwa kwa kuchangia katika ukosefu wa ajira na kuzidi kwa uhalifu nchini humo.
Raia 21 wa Afrika Kusini ni kati ya wale waliouawa, baada ya kudhaniwa kwamba walikuwa ni wageni.

Thursday, August 14, 2008

AGOSTI 15, 2008 MAISHA YANGU


Kila nikiwaza sipati jibu, kwani maisha yangu ni tofauti sana na ndugu zangu. Mara nyingine naona kama nimetokea hewani (yaani sina ndungu na pia sina mama wala baba) niliondoka nyumbani mapema. Nikiwa na miaka 16, nilianza kujitegemea mapema sana kuliko ndugu zangu. Sijaishi sana na wazazi wangu na sijawategemea sana. Sijafaidi kuwa mtoto wao kama mwenzangu. Na pia sijawategemea sana kwa jambo la uchumi ila kwa namna nyingine. Yaani kama nilivyokuwa shuleni nilipata pesa za matumizi labda kama 200-500Tsh, na hiyo ilikuwa ni matumizi ya mwezi mzima au zaidi. . Wakati nilikuwa mdogo nilikuwa na kanga upande mmoja, vyupi viwili, magauni mawili moja la kuchezea na moja la jumapili. Nilikuwa narithi magauni ya mama, anapunguza na ananishonea mimi. Viatu nilikuwa nasikia jina tu nikipata ndala (za matairi ya gari) nilikuwa najisikia kweli. Fikiria mwenyewe kwenda mstuni kutafuta kuni bila viatu. Unachomwa na miba, unaweza kukanyaga nyoka n,k. Sio kusema wazazi wangu hawakuwa na uwezo hapana. Ila hawakuona kama ni muhimu watoto kuwa na vitu vingi. Pia nilipokuwa mdogo mambo ya kunywa soda, kula pipi hayakuwa kabisa kichwani mwangu. Kwani hatukuzoeshwa Sio kusema maisha yangu yalikuwa mabaya hapana. Mahitaji muhimu nilipata kama kawaida. Lakini sasa watoto wengi hawaridhiki na gauni/shati au suruali moja. Pia wanataka viatu. Na halafu wanataka kila mtu na chumba chake cha kulala. Mimi nilikuwa nanalala chumba kimoja na kitanda kimoja na kaka yangu . Kila mtu alionyesha kichwa upande wake. (mzungu wa nne) Lakini leo mdogo/ndugu zangu wana karibu kila kitu. Kwa jambo hili mara nyingi najisikia nipo peke yangu hapa duniani.

Maisha yangu kwa ujumla hayajawa rahisi. Kipindi kile nasoma kuwa karani nilipata shida sana mimi, asubuhi nilikuwa naamka kuandaa chai na baadaye kwenda shule kwa mguu labda kama saa moja au dakiki 45 hivi. Mchana nilikuwa nabaki shuleni, kwani mwanzoni nilikuwa narudi na sikupata chakula. (Bali ilikuwa kwenda kuchota maji unajua tena foleni kubwa.) Niliporudi na maji kuanza kuandaa chakula, na baadaye muda wa kurudi shuleni umefika. Basi ni kugeuza tena tu bila kula kwani ningekula basi ningechelewa. Nilikuwa naishi kwa "ndugu" lakini nilikuwa kama MFANYAKAZI (mama wa nyumba alikuwa mkatili mno sio mchezo). Jioni baada ya shule kufika tu bila kula kitu amekwishaandaa mahindi kwenda kusaga na niliporudi tu ni kuchukua ndoo kwenda kuchota maji na pia kuandaa mboga. Usidhani hapakuwa na watoto wao, walikuwepo. Lakini walikuwa wanacheza, kufanya homework au walikaa tu. Kila siku hivyohivyo kwa muda wa miaka 2. Labda ndio maana maisha yangu sio kama ndugu zangu, na ndio maana sikuweza kufanikisha masomo yangu vizuri. Kwa namna nyingine namshukuru (mama wa nyumba) amenifundisha jinsi ya kujitegemea, kuishi peke yangu. Ila jamani tembeeni mwoone mmh maisha ni safari ndefu.

Agosti 14, 2008 MASHAIRI

MAPENZI
Mapenzi, mapenzi, mapenzi,
Ingekuwaje bila mapenzi,
Bila mabusu na kupapasana?
Mimi nakuwaza wewe tu,
Mikono yako wakati unaponigusa,
Macho yako na mikono yako unapotabasamu,
Maisha yanapendeza,
Mpenzi, nikumbatie mimi na sema ya kuwa unanipenda.

WEWE
Wewe mpendwa, wewe ni maisha yangu,
Ambaye nataka kuishi naye,
Katika ndoto zangu, katika ndoto za maisha nakushona na uzi wa dhahabu,
Rohoni mwangu, upo wewe na mimi, tumefungwa katika nyavu.

2008,8,14 UTAJIRI WA LUGHA

Watanzania kwa kweli tuna haki ya kujivunia nchi yetu nzuri yenye amani na utulivu. Halafu sasa kitu kinachonifurahisha ni kwamba Tanzania haina utajiri wa mbuga za wanyama tu na mlima wetu mrefu Kilimanjaro ambavyo watalii huja kuangalia. Hapana, Tanzania ni tajiri wa lugha mnajua hakuna nchi yenye makabila mengi kama TZ. Makabila 129(130) ambayo ni machache tu huwa wanaelewana wanapoongea, kama vile Wangoni na Wamanda, Wabena na wahehe nk. Hii ndiyo maana Hayati baba wa Taifa Mwl. J.K Nyerere aliona ni vema kuwe na lugha moja ambayo watu wote tutaweza kuongea na kuelewana ni lugha ya Taifa KISWAHILI.

Wednesday, August 13, 2008

AGOSTI 13, 2008 MADAWA YA KULEVYA

Duniani wote tunapenda sana kijisikia vizuri. Tunataka kujisikia kuwa na raha, wenye nguvu na sio kuwa na wasiwasi. Hivyo wengi wetu tunaanza kufikiria kuwa dawa za kulevya, pombe na sigara zitatupa raha. Angalia sana! usidanganyike! kutumia vitu hivyo ili kupata furaha bali ni kuhatarisha maisha kwani unaweza kujikuta umeingia ulevini. Kujinasua kwenye hali hiyo itakuwa kasheshe kwelikweli (si lelemama) inahitaji moyo na pia kujizatiti.


Leo nimejisikia kuandika kwa kiswidi pia ili nao wafurahi:

LIVSSTILSHOT
Tobak är gift för kroppen
Rökning är extremt skadlig och ökar risken för cancer, sjukdomar i luftvägarna, hjärt-kärlsjukdomar, typ 2- diabetes, magsår, benskörhet, nedsatt fruktsamhet och dålig sårläkning. Tobaksrök innehåller över 4000 olika ämne, varav många äa giftiga - till exempel koloxid och nikotin - medan en del är tjärämnen och andra partilar som sätter sig i luftvägarna.
Alkohol ger organskador
Alkohol i en mängd överstigande 15ml ren alkohol per dag är skadlig för bukspottkörtel, tarm, lever samt nervcellerna i hjärnan och andra ställen i kroppen. Organskadorna kan leda till dåligt upptag av vitaminer och mineraler, viliket i sig påverkar hälsan negativt. Alkoholens skadeverkningar beror på att det är ett lösningsmedel som irriterar cellerna och belastar leve.

Tuesday, August 12, 2008

AGOSTI 12,2008 RAHA YA KUWA NA MISITU

UYOGA




BLUEBERRY
Raha ya kuwa na misitu leo nimeenda msituni nimachuma uyoga pia blueberry(samahani naomba msaada sijui blueberry ni nini kwa kiswahili.

AGOSTI 12,2008 URAFIKI, MAPENZI NA NDOA

Mara nyingi nimekuwa nimejiuliza:- Hivi maisha yangekuwa vipi kama kusingekuwa na urafiki? Rafiki si mtu tunayecheka na kufurahia naye maisha tu, hapana bali pia tunayekuwa naye katika shida na raha! Marafiki hutusaidi kupata majibu ya maswali mbalimbali yanayotukabili. Katika ndoa, urafiki ni msingi imara kwani wanandoa wanatakiwa kuwa marafiki. Lakini hata hivyo bado sijapata jibu sawa sawa kuwa rafiki wa kweli ni nani? na anatakiwa kuwa na sifa gani?

Monday, August 11, 2008

AGOSTI 11,2008 LUNDO, KUMBUKUMBU

Leo nimekumbuka sana Lundo, eeh jamani ilikuwa kazi kweli. Wale wote waliofika Kijiji cha Lundo Tanzania. Yaani pale Lundo shule ya msingi ya wakimbizi kwa sasa inaitwa Lundo Secondary School.

Mnajua pale shuleni kulikuwa na matunda ya aina mbalimbali kama vile mapapai, machungwa, malimao, ndizi n.k. Na mimi ilikuwa kazi yangu kila baada ya shule nilirudi tena shuleni, nilikuwa mwizi wa malimao nilikuwa nakula sana malimao kwa siku nilikuwa nakula 10. Mama alikuwa analalamika sana. Kwani nilikuwa nakula na chumvi iliyochanganywa na pilipili. Nilikuwa siibi malimao tu chumvi pia.

Halafu magauni yangu na sketi zilikuwa na matobo sana, sababu nilikuwa nabebea malimao. Mmh! jamani Lundo sitasahau, yaani kujificha kwa kweli nilikuwa mwizi maalufu kwani sikushikwa. Ila sasa siwezi kula malimao zaidi ya nusu limao nimekinai kabisa.

LUNDO BAADA YA MIAKA ISHIRINI
Mmhh furaha, hisia pia raha vilinijia siku hii yaani mwaka jana 2007. Fikiria mwenyewe sehemu uliyozaliwa, sehemu ulianza darasa la kwanza halafu umeondoka na baada ya miaka 20 unarudi/tembelea tena.
Ila nilisikitika kidogo kwani sikuweza kujua ni nyumba gani nilizaliwa/ishi kulikuwa na mabadiliko mno. Ila cha kufurahisha zaidi ni kwamba nilionana na mjomba wangu ambaye sikumwona tangu 1985. Siku hii nilikuwa kama mtoto mdogo nilikimbia na kumrukia mjomba kwa jinsi nilivyokuwa na furaha. Mpaka machozi yalinitoka. Kwa vile mjomba anajua mimi napenda nini aliniandalia samaki What a joy. pia nilifurahi zaidi kujua alikumbuka jina langu la utani ambalo hata mwenyewe nilisahau. Mnataka kujua au? Okey ni (KANYANJA) kilugha kiswahili kanyasa. Sasa mnajua .

Sunday, August 10, 2008

AGOSTI 10,2008 KUMBUKUMBU

Angekuwa sweden huyu angaumia kweli na baridi.Kwani hapa wakati wa joto ni kama makambako.

Saturday, August 9, 2008

AGOSTI 9,2008 MIMI YASINTA

Leo, kuna jua kidogo nimeamka nimevaa nguo zangu za mazoezi na kuanza kukimbia baada ya kukimbia kidogo mvua hiyo lakini kwa vile nilishaamua kukimbia basi nimeendelea nimekimbia kilimeta 5. Ila sasa nimerudi na natetemeka kama kifaranga cha kuku. Nataka nifanye mazoezi ili niiwakilishe Nchi yangu Tanzania kwa jinsi ninavyoipenda. Mnajua hii hali ya hewa ya hapa inaniuzi sana kwani kila siku hali nyingine leo jua kesho mvua keshokutwa baridi na hata pengine theruji hakuna msimamo. Kwa hiyo kama hujitosi tu kukimbia au kuwa mstuni labda kutafuta uyoga au matunda basi utabaki ndani ya nyumba siku hadi siku.

Mnajua leo nimekumbuka sana nyumbani kwa hiyo nimeamua kupika ugali na mchicha pia maharage. Nimeukanyaga kweli lakini hata hivyo haitoshi kwa hiyo nimeamua kusikiliza mziki.

Friday, August 8, 2008

8,8 .2008 SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE








Mwenzenu nilisahau kabisa kuwa leo ni sikukuu ya nane nane. Kuna rafiki kanikumbusha asante sana kwani bila wakulima hatungekula.

Thursday, August 7, 2008

AGOSTI 7,2008 THE KONDOA-IRANGI ROCK PAINTING

Hapa ilikuwa zamani za kale kule Kondoa baina ya Singida na Irangi Hills. Ni baina ya miaka 19000 na 30000 iliyopita babu zetu walikuwa wakichoro kwenye mawe safi eeeh.

AGOSTI 7,2008 NYWELE




The Sixties were the era of long hair.As long as the hippies were wearing their hair long and bein' against war and stuff, Black people decided they wanted to do it, too. Hippy hair hung down, Black people's hair went in every direction. This was known as the Afro.
This looked so neat that white people started getting perms so they could have Afros, too. But then Michael Jackson turned white, so Black people decided maybe they'd do corn rows instead.

Wednesday, August 6, 2008

Agosti 6, 2008 KIJIJI CHA IFINGA

Mpunga


Kanisa

Najua wote mtashangaa sawa mnaruhusiwa kushangaa. Kwani mimi leo nimetembelea kijiji kimoja kiitwacho Ifinga, Kijiji hiki ni maalufu sana kwa kilimo cha mpunga. Kwa hiyo ukifika/tembea Ifinga chukua na unga wako usije ukatamani ugali kwani wao wanakula wali kila siku siku wanayokula ugali ni sikuuu au jumapili tu.

Tuesday, August 5, 2008

AGOSTI 5,2008 AFYA

Mwenzenu nahisi kuchanganyikiwa. Labda kwa sababu nina tamaduni/mila na desturi mbili najua mimi ni mtanzania na najua mila na desturi pia utamaduni wangu. Lakini sasa kichwa/akili yangu imevurugika kabisa:-

Ni hivi najua nyumbani TZ ni kawaida au labda niseme safi kama mtu umenenepa/nawili. Nakumbuka mwaka wa kwanza niliporudi TZ kusalimia watu walishtuka/shangaa sana na kuzani nilikuwa na ngoma au. Na baada ya miaka kadhaa nikarudi tena na wote walifurahi na kusema ya kwamba hivi ndiyo inavyotakiwa, wao walisema ya kwamba nilipendeza yaani niliongoza kilo kidogo nilinenepa. Na niliporudi hapa watu walisema eeh? Mbona unanenepa sana si vizuri inabidi upungue. Sasa nadhani mmegundua kwa nini nimesema nimechanganyikiwa. Ngoja niendelee kidogo kiundani au niseme kiafya nakubaliana na "waswidi" wazungu, lakini hali hii inanipa hofu kidogo kwani sasa hata watoto wadogo wanafuata mwenendo wa wazazi na marafiki pia, wanajinyima kula. Na wengine wanakula kama kawaida na baadaye wanatapika makusudi. Mnajua wanasemaje, eti wanataka kuwa wembamba, ndiyo wanapendeza. Lakini ukiwaangalia wanaonekana kama mti hata matako (wowowo) hawana.
Ndiyo najua kunenepa sana sio safi kwani kuna madara yake kama vile mshtuko wa moyo(heart attack) daibetes nk.

kama nilivyosema hapo juu mara nyingi sijui mimi ni nani na nchi gani ni yangu. ndio maana nimesema nimechanganyikiwa. Watanzania (waafrika) wanaona kunenepa ni safi na wazungu wanasema ni hatari, Na najua hakuna anayesema kweli au uongo. Je wasomaji mnasemaje Nisaidieni kidogo!!!!!!!!!

Monday, August 4, 2008

Agosti 4, 2008 SAMER/WAMASAI



Hapa nataka kusema sio wamasai tu wanaishi kwenye nyumba kama hizi manyata kwani hata hapa Sweden kuna watu aina ya wamasai wanaitwa Samer wao ni maalufu sana kwa kufuga (rendeer) kulungu kwani wao wanaishi sehemu ya baridi sanaaaa. Na wamasai wetu wote tunajua maalufu kwa ufugaji wa ngómbe.

Saturday, August 2, 2008

AUGOSTI 2, 2008 HALI YA HEWA NYUMBANI SONGEA

Kama mnataka kuangalia hali ya hewa Songea Bonyeza hapa

AUGOSTI 2, 2008 UTANI

Kuna watu wengi wanapenda sana mambo ya utani kiasi kwamba yule anayempa ule utani anaami ni au anaweza mpaka kuchanganyikiwa. Mimi mwenyewe ni moja wa watu hao, napenda sana utani laki ni sio kwamba nataka kuwatesa au kuwachanganya la hasha. Ninachotaka kusema hapa ni kwamba kama ule utani umepita mipaka na unakaribia kuwapoteza marafiki zako wote utafanyaje. Kwani hilo swali nimepata leo kwa rafiki mmoja amemdanganya rafiki yake kwamba wakutane sehemu furani lakini kumbe ni uwongo je afanyeje ili wawaze kuwa marafiki tena. Kwani anajisikia vibaya pia anaona aibu kwa kuwa mwongo. Hataki kumpoteza rafiki yake kwani ni mabest. Pia anasema kwa vile wako mbalimbali kama ingekuwa karibu angejaribu kuongea naye na kuomba radhi. Kwa yeye aliona kama ni mchezo. Wasomaji naomba mnisaidia nimwambieje huyo ili amwambie rafiki yake wa mbali.