Saturday, February 11, 2017

SIKU MBAYA (Jifunze kupitia simulizi hii)

Nimeamka asubuhi hii na kukutana na simulizi hii katika barua pepe yangu. Baada ya kusoma nikaona ni simulinzi nzuri na ya kufundisha  katika maisha ya kila mwanajamii. Kwa hiyo nikaona niiweke hapa kibarazani kwetu ili  kwani elimu hawanyimani...karibuni 
Kijana akiwa katika maombi
Ilikuwa ni saa moja na nusu saa za asubuhi ambapo kijana aitwae John alikuwa ndo anaamka.
Mara baada ya kuamka na kukamilisha ratiba yake ya asubuhi ikiwemo kuoga, kupiga mswaki na kupata kifungua kinywa kijana alienda alipopaki gari yake tayali kwaajili ya kuelekea ofisini. Ile anataka kuwasha gari yake ghafla engine ikagoma kuwaka. Akashuka kwenye gari yake na kuamua ketembea kwa miguu mpaka kituo cha mabasi. Hata hivyo baada ya kufika kituo cha mabasi hakufanikiwa kupanda basi kwa kuwa mabasi yote yalikuwa yamejaa.

Ili asichelewe kazini kijana akaamua kukodi tax. Akiwa ndani ya tax alipigiwa simu na mmoja kati ya washirika wake kibiashara lakini kabla hajapokea simu ikazimika na hata alipojaribu kuiwasha akagundua betri ilikuwa imekufa. Akiwa bado yupo ndani ya tax mwendo kidogo baadae tax nayo ikazimika ghafla na haikuweza kuendelea na safari. Akamlipa dereva tax pesa yake na kuamua kukodi tena pikipiki (bodaboda) ambayo ilimfikisha mpaka kazini kwake. 

Kabla hajaingia ofisini kwake mtu mmoja akataka kumshika mkono na kumpongeza kwa promotion ambayo ilitakiwa kufanyika siku hiyo.
Lakn kabla hajafanya hivyo akaitwa na mtu kwa nyuma ambaye baadae akamwambia kwamba promotion ilikuwa imeahilishwa.

Jioni baada ya kufika nyumbani kijana akaanza kunung'unika huku akisema:
"mambo gani haya!!!"
"kwanini leo imekuwa SIKU MBAYA kwangu kiasi hiki!!"
"Ee Mngu nimekukosea nini mimi mpaka siku yangu iwe mbaya kiasi hiki!!" 
Mara ghafla akasikia sauti ya Mumgu ikisema:
"Asubuhi ulipowasha gari yako ikagoma kuwaka mm nilihusika kwa sababu ungepata ajali mbaya sana kama ungetoka na gari yako leo"
Ulipotaka kupokea simu betri ikafa mm nilihusika kwa sababu aliyekupigia simu alitaka kukupatia taarifa za uongo ambazo zingepelekea kuharibu uhusiano kati yako na wafanyabiashara wengine.

Hatua chache baadae tax ilishindwa kuendelea na safari kwa sababu yule dereva tax ni agent wa kikundi cha wateka nyara hivyo kama mngeenda mbele zaid huko angebadili mwelekeo na kukupeleka chini ya jengo moja kubwa ambalo limekuwa likitumika kwa shughuli zao za uharifu na hatimae wangekuteka.

Ulipofika ofisini nilizuia mtu mmoja asikushike mkono kwa sababu nilikuwa nakuepusha na maambukizi ya ebora kwani yule mtu amesha ambukizwa vurusi vya ugonjwa huo

Baadae kidogo ile promotion ambayo ulitegemea ikuingizie pesa nyingi sana ukaambiwa imeahilishwa hapo napo mimi nilihusika kwa sababu kuna mtu hakufurahia ww kupata nafasi ile hivyo akaamua kupandikiza mapepo kwenye kiti ulichotakiwa kukalia ndani ya ukumbi ambapo mapepo hayo yangepelekea kifo chako.

Sasa hebu niambie 
-Siku ya leo ilikuwa mbaya kwako
-Na je yote niliyokutendea yalikuwa mabaya?Kijana kusikia hivyo alilia sana,akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung'unikia Mungu. Akapiga magoti akatubu,  hukuakimshukuru Mungu.
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Ninachotaka hapa uelewe ni kwamba upo hai leo ni kwa sababu Mungu amependa uwe hai na ana makusudi na maisha yako.

Wakati mwingine kuna mambo mabaya huwa yanatokea katika maisha yetu yanayotufanya tuone kama Mungu ametusahau.
Tunamnung'unikia na kumlaumu Mungu bila kujua kuwa Mungu ana njia nyingi sana za kutuepusha na mabaya.
Wakat mwingine tunasahau kuwa mabaya tunayokutana nayo yanafanya kazi kwa Manufaa ya hatma zetu.

Unaweza fukuzwa kazi usijue kumbe ndio unaelekea katika kazi bora zaidi,
Unaweza kuachwa na mtu uliyempenda sana ukadhani ndiyo mwisho wa maisha kumbe Mungu amekuandalia mtu mwingine mwenye mapenzi ya dhati mtakayefikia malengo ya kujenga familia,
Unaweza kukataliwa na kutengwa na ndugu kumbe Mungu amekuandalia watu-baki watakaofanikisha ufikie malengo yako pasipo masimango ya ndugu,
Unaweza kuona marafiki wanakusariti kumbe Mungu anawaondoa makusudi ili kukuepusha na mabaya waliyoyapanga juu yako.  

MWISHO naomba nikuhakikishie kwamba Mungu anayaona matatizo yako na kwa hakika hatoacha yakuangamize bali atakwenda kufanya njia ya kutokea ktk magumu yote unayopitia.
Kama unaamini kwanini usiseme AMEN.

No comments: