Tuesday, August 29, 2017

HISTORIA FUPI YA WANGONI WAKIWA KATIKA ARDHI YA WASHONA WAKIJA KATIKA ARDHI YA TANZANIA

Historia ya Afrikas foto.

Mara baada ya kutokea vita vilivyofahamika kwa jina la mfekane kwenye miaka ya 1800, , vilivyokuwa vikihususisha makabila yalikuwa yakipatikana kusiniu mwa Afrika. Wangoni waliamua kuondoka na kusambaa Afrika mashariki na kati wakiwa na Kiongozi wao Zwangendaba. Wakati wanasambaaa Afrika mashariki na kati, Wangoni walipitia sehemu nyingi sana, zipo sehemu walizopokelewa kwa heri na zipo sehemu walizopokelewa kwa shari. Lakini ukweli ni kwamba Wangoni waliondoka Afrika kusini kutokana na vita vilivyotokea. Na sababu kubwa ya vita hivyo ni sera ya upanuzi ya mfalme wa kabila la Wazulu aliyefahamika kwa jina ka Tshaka Zullu. Kutokana na vita hivyo ambavyo pia vilihusisha hata watu wengine ambao hawakuwa Waafrika kama vile Wadachi na Waingereza. Hivyo Wangoni waliamua kuondoka kusini mwa Afrika na kuja Afrika ya mashariki na kati. Sasa wakati wanakuja Afrika ya kati na mashariki Wangoni walipita sehemu nyingi sana. Moja ya sehemu ni ardhi ya Washona . Kwa ufupi ni kwamba Washona ni moja ya jamii zinazopatiakana katika ardhi ya Zimbabwe. Na zaidi jamii ya Washona wanapatikana mashariki mwa jamii za Wakalanga ( hii ilikuwa moja ya sehmu ambayo Wangoni walipita mara baada ya kuvuka mto Limpopo). Washona waliamia maeneo hayo wakiongozwa na mtemi wao aliyefahamika kwa jina la Ska-vunza kwenye karne ya 18. Na ifahamike kuwa Washona ni moja ya kabila ambalo linapatiakna katika kundi hili la Wangoni.