Tuesday, April 10, 2018

VYAKULA VYA USWAHILINI VINAVYOSAHAULIKA

Naanza kuwaza hili jambo iweje tusahau vyakula kama hivi vilivyotukuza, au ndo kama vile tunavyopenda mavazi ya kigeni na sasa ipo kwenye vyakula pia?

4 comments:

Rachel Siwa said...

tunapotea au tunajipoteza nafikiri...

Yasinta Ngonyani said...

Kachiki wa mimi upo sahihi twajipoteza na hasa kwa kupenda kuiga

ray njau said...

Asanteni sana akina mama wapendwa Rachael& Yasinta kwa maoni yenu chanya.Utafiti usio rasmi sana unaonyesha kuwa ongezeko la magonjwa ya kisukari na mengineyo ni watu kusahau au kuacha kabisa kula vyakula vya asili vilivyowapatia makuzi.
Ubadilishaji ghafla aina za mifumo ya maisha ndiyo athari tokezi katika mizoroto ya kiafya kupitia magonjwa yasiyo na maambukizi.
Kule uchagani tulikula somi tsa mmbala(kunde+magadi),kyumbo( mchanganyiko laini wa ndizi+kunde+magadi),kitawa( mchanaganyiko laini ndizi+maziwa) ngararimo(mahindi makavu+kunde+magad, mtori(mchanganyiko alini wa ndizi na nyama)
Michanganyiko hiyolaini hunywea ingali moto kwa kutumia(mboriko) vibakuli vya miti.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Njau! yaani ww acha tu ni masikitika kuona /kusikia watu/jamii asilia kubwa wameaacha kula hivyo vyakula vya asili bila kugundua ukasi wa magonjwa tupatayo.
Itabidi nije huko kula hivyo vyakula vitamu na vya asili